JK akumbushwa kutangaza mali alizochuma kabla ya kung'atuka.
Mkurugenzi wa Idara ya Utetezi na Maboresho kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia, amemkumbusha Rais Jakaya Kikwete, asiondoke kimyakimya bila kutangaza au kuorodhesha mali alizochuma wakati akiwa madarakani.
“Rais Kikwete alijaza fomu ya mali alizokuwa nazo Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, lakini hakutangaza. Tunasubiri kuona sasa baada ya kumaliza atatangaza mali aliyopata akiwa madarakani,” alisema.
Alisema mwaka 1995, Rais mstaafu,...
Vijimambo