Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


MAJANGA TENA; MZEE SMALL AFARIKI DUNIA

Muigizaji mkongwe nchini, Said Ngamba maarufu kwa jina la Mzee Small amefariki dunia usiku huu akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar. Mzee Small amefariki kwa ugonjwa wa presha baada ya kuugua kwa muda mrefu kabla ya kuzidiwa jana na kupelekwa Muhimbili. Mtoto wa marehemu aitwaye, Muhidin amethibitisha kifo cha Mzee Small. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!… ...

GPL

Read more


Habari Zinazoendana

11 years ago

Michuzi

BREAKING NYUZZZZZ.....: MZEE SMALL AFARIKI DUNIA USIKU HUU

MUIGIZAJI MKONGWE HAPA NCHINI,SAID NGAMBA MAARUFU KWA JILA LA MZEE SMALL AMEFARIKI DUNIA USIKU WA LEO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI ALIKOKUWA AMELAZWA AKIPATIWA MATIBABU.
AKITHIBITISHA TAARIFA YA KIFO CHA MZEE SMALL,MWANAE AITWAE MAHMOUD AMESEMA MZEE WAKE AMEFIKWA NA MAUTI HAYO MAJIRA YA SAA NNE USIKU WAKATI AKIWA HOSPITALINI HAPO AKIENDELEA KUPATIWA MATIBABU.
MIPANGO INAFANYIKA NYUMBANI KWAO TABATA NA KADRI TAARIFA ZITAKAVYOKUWA ZIKITUFIKIA TUTAENDELEA KUJULISHANA.
NI PIGO...

 

11 years ago

Bongo Movies

SAD News: Muigizaji Mkongwe Nchini Mzee Small Afariki Dunia.

Mwigizaji maarurfu nchini Said Ngamba "Mzee Small" amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kupatwa na pressure na kukimbizwa hospitali ya taifa Muhimbili. Muigizaji huyo mkongwe kabla ya kifo chake aliugua kwa muda mrefu pia. Mzee Small ni mmoja wa wasanii wa mwazo katika sanaa ya maigizo nchini kwenye enzi zake akiwa ametamba na wasanii wenzake wakongwe kama vile Bi.Chau na King Majuto, ni mmoja wa wasanii ambao mchango wake katika sanaa ya maigizo na tasnia ya filamu nchini hauwezi...

 

10 years ago

GPL

MZEE OJWANG AFARIKI DUNIA

MWIGIZAJI nguli raia wa Kenya, Benson Wanjau 'Mzee Ojwang' amefariki dunia jana jioni akiwa Hospitali ya Taifa ya Kenyatta, alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu (Pneumonia). Mzee Ojwang atakumbukwa katika Vipindi vya Televisheni kama Vitimbi, Vioja Mahakami, Vituko na Kinyonga. Amefariki akiwa na umri wa miaka 78.

 

11 years ago

GPL

MZEE GURUMO AFARIKI DUNIA

Maalim Muhidin Gurumo enzi za uhai wake. MKONGWE wa Dansi nchini, Maalim Muhidin Gurumo aliyekuwa akitumikia Bendi ya Msondo Ngoma ‘Baba ya Muziki’ kabla ya kustaafu mwaka jana, amefariki  dunia. Kwa mujibu wa habari tulizozipata kupitia chanzo chetu, Mwanamuziki huyo amefariki alasiri hii katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matibabu. Mpaka sasa sababu ya kifo cha Mzee Gurumo bado...

 

11 years ago

GPL

MZEE DUDE AFARIKI DUNIA

Mzee Dude enzi za uhai wake. MSANII wa kundi maarufu la vichekesho na uigizaji la Futuhi, Mzee Dude amefariki dunia akiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando iliyopo jijini Mwanza leo jioni! Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.…

 

10 years ago

CloudsFM

MSANII MZEE MANENTO AFARIKI DUNIA

MSANII wa filamu za Kibongo, Mzee Manento amefariki dunia jana jioni kiwa jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa moyo.
Mzee Manento atakumbukwa katika filamu alizocheza kama 'Hero of the Church', 'Dar to Lagos', 'Fake Pastor' na nyinginezo.

 

10 years ago

Dewji Blog

Mzee Ebby Sykes afariki dunia

Sykes+3

Baba mzazi wa msanii mkongwe wa muziki nchini, Dully Sykes, Mzee Ebby Sykes amefariki (pichani) dunia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa binti yake Raya Sykes amethibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram.

Raya katika ukurasa wake huo aliandika ‘Mungu akulaze mahala pema peponi baba angu mimi nilikupenda lakini Mungu alikupenda zaidi….nasikitika nipo mbali sitaweza kukuzika. Ulikuwa ni mtu mwenye upendo na kila mtu alikupenda, nakupenda sana baba...

 

10 years ago

Vijimambo

MZEE PETER KISUMO AFARIKI DUNIA

Muasisi wa Tanu na baadaye CCM, Mzee Peter Kisumo (pichani) amefariki dunia. Mwanasiasa huyo mkongwe nchini ambaye aliwahi kushika nyadhifa kadhaa katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, alifariki Dunia jana saa moja usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.Mtoto wa marehemu, Michael Kisumo alilithibitishia juu ya kifo cha baba yake akisema kilitokana na maradhi ya figo ambayo yamekuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.

“Tulikuja hapa Muhimbili kwa ajili ya mzee kufanyiwa dialysis (usafishaji damu...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani