Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Ajali ya basi yaua mmoja, yajeruhi 46

NA ABDALLAH AMIRI, IGUNGA

MTU mmoja, amefariki dunia papo hapo na wengine 46 kujeruhiwa vibaya baada ya basi la Kampuni ya ALLY’S lenye namba za usajili T 560 AKW aina ya Scania, kupinduka katika Kijiji cha Igogo, Kata ya Nanga, Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora.

Ajali hiyo ilitokea jana, saa 12 alfajiri wakati basi hilo lilipokuwa likitoka wilayani Igunga kwenda jijini Mwanza.

Wakizungumza na MTANZANIA eneo la tukio baada ya ajali hiyo, mmoja wa abiria aliyenusurika, Emmanuel Julius (32),...

Mtanzania

Read more


Habari Zinazoendana

11 years ago

Habarileo

Ajali ya basi yaua 10, yajeruhi 30

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Charles MkumboWATU 10 wamekufa papo hapo na wengine 30 kujeruhiwa vibaya kutokana na ajali ya basi la Luhuye Express lililokuwa likitoka wilayani Tarime mkoani Mara kwenda jijini Mwanza jana.

 

10 years ago

Mtanzania

Ajali nyingine yaua mmoja, yajeruhi 28

air jordanNa Thomas Murugwa, Tabora
BASI la Kampuni ya Air Jordan lenye namba za usajili T 650 AQZ lililokuwa likitokea Mwanza kuelekea Arusha, limepata ajali katika Kijiji cha Ngonho, Kata ya Kitangili, Wilaya ya Nzega mkoani Tabora na kusababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi 28.
Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Jackline Liana, imemtaja aliyefariki dunia kwa jina moja la Emmanuel ambaye alikuwa ni fundi wa gari hilo.
Alisema sababu ya ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva ambaye jina...

 

10 years ago

GPL

AJALI YA BASI LA SUPER FEO YAUA 3, YAJERUHI 28 MKOANI MBEYA

WATU watatu wamekufa papo hapo huku wengine 28 wakijeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Super Feo walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mbeya kwenda Songea mkoani Ruvuma kupinduka na kutumbukia mtoni leo asubuhi. Ajali hiyo imetokea katika Kijiji cha Shamwenga, Kata ya Inyara mkoani Mbeya.

 

10 years ago

GPL

AJALI YA BASI LA SIMBA MTOTO NA FUSO YAUA MMOJA

Fuso likiwa limeharibika vibaya baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Simba Mtoto. Basi la Simba Mtoto baada ya ajali.…

 

10 years ago

Habarileo

Ajali yaua 2 yajeruhi 45

David Misime.WATU wawili wamekufa papo hapo huku wengine 45 wakijeruhiwa baada ya basi la abiria lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Mwanza kugongana uso kwa uso na roli katika kijiji cha Vikonje wilayani Chamwino mkoani hapa.

 

11 years ago

Tanzania Daima

Ajali yaua 6, yajeruhi 12 Dar

WATU sita wamefariki dunia papo hapo na zaidi ya 12 kujeruhiwa katika ajali mbaya iliyohusisha magari manne. Akizungumzia tukio hilo lililotokea jana eneo la Makongo, jijini Dar es Salaam, Kamanda...

 

10 years ago

GPL

AJALI YAUA WAUJAJI 17 , YAJERUHI 27 NEPAL

Taswira kutoka eneo la ajali. MAUJAJI 17 wa dhehebu la Kihindu kutoka India wamepoteza maisha leo katika ajali ya basi walilokuwa wakisafiria katika Wilaya ya Dhading karibu na Mji wa Kathmandu nchini Nepal. Katika ajali hiyo, maujaji 27 wamejeruhiwa huku watano kati yao wakiripotiwa kuwa katika hali mbaya, Ubalozi wa India nchini Nepal umeeleza. Basi hilo lilikuwa likitoka Kathmandu kwenda Mji wa Gorakhpur. Maujaji hao walikuwa...

 

10 years ago

Habarileo

Ajali yaua 4 Moshi, yajeruhi 3 Handeni

Lori likiwaka moto wilayani Handeni.WATU wanne wamekufa na watatu wamejeruhiwa katika ajali mbili tofauti, zilizotokea Moshi mkoani Kilimanjaro na Handeni mkoani Tanga.

 

11 years ago

GPL

AJALI YAUA 6 TANGA, YAJERUHI ZAIDI YA 12

WATU sita wamefariki papo hapo na zaidi ya 12 kujeruhiwa baada ya gari la abiria aina ya Toyota Hiace kuligonga kwa nyuma lori la mizigo lililokuwa limeharibika barabarani bila kuonyesha ishara yoyote eneo la Kange jirani na mizani mkoani Tanga! Baadhi ya majeruhi katika ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mkoa Tanga kwa matibabu!

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani