Jifunze Kiswahili Fasaha
Ningependa kuwauliza wasomaji wangu  kwa nini waandishi hawazingatii maelekezo na maoni  yanayotolewa mara kwa mara katika gazeti hili kuhusu uandishi bora. Inawezekana kuwa baadhi ya waandishi hawa hawasomi makala zangu ama hawayaelewi au hawapendi kujifunza. Hata hivyo, hatutakata tamaa kwani taaluma ya saikolojia inadai kuwa wako watu wenye vichwa vigumu kuelewa jambo na wako wengine wepesi kukubali mabadiliko.
Mwananchi
Habari Zinazoendana
9 years ago
Mwananchi02 Nov
Misingi ya Kiswahili Fasaha
Kwa bahati mbaya sana wanaosoma makala zangu na kuleta mrejesho ni wasomaji wachache tena ni wa kawaida tu. Hajatokea mwandishi wa magazeti au hata mhariri anayejali kusoma kwa makini ili kutoa maoni yake kwa lengo la kuyakosoa maoni ninayotoa kwa lengo la kuchangia mawazo. Makosa mengi ninayoyaona yanajirudia mara wa mara na hata baada ya kuyatolea ufafanuzi sijaona maendeleo yanayojitokeza. Hii ni dalili tosha kuwa baadhi ya waandishi na watangazaji hawasomi maoni haya na kama wanasoma...
9 years ago
Mwananchi19 Oct
Kiswahili sanifu na fasaha
Mnamo mwaka 1968 Mwalimu Julius K. Nyerere aliwahi kusema kuwa elimu inayotolewa haina budi kumchochea mtu kuwa na mambo yafuatayo: Kwanza ni kuwa na akili yenye udadisi wa mambo. Pili ni kuwa na uwezo wa kujifunza kutokana na yale yanayofanywa na wengine. Tatu ni kujiamini kama mtu huru aliye sawa na wengine katika jamii. Nne ni kuthaminiwa na wenzake kutokana na matendo yake na wala siyo kile alichonacho.
11 years ago
Mwananchi16 Feb
Kiswahili fasaha kitumike Bunge la Katiba, siyo ‘Kiswanglish’
Hivi karibuni Mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba (jina limehifadhiwa) aliwahi kuhojiwa na mwandishi wa makala haya kuhusu matarajio ya Watanzania kuhusu Katiba Mpya na matumizi ya Kiswahili.
10 years ago
Mwananchi30 Apr
Jifunze Kiswahili
Ni mara chache tunasoma makala au taarifa katika magazeti na pia katika majarida na kujiridhisha kuwa muundo na mpangilio wa maneno unakuwa fasaha na sanifu. Kinachoonekana ni ukosefu wa umakini katika matumizi, maana na tahajia sahihi za maneno.
9 years ago
Mwananchi17 Dec
Jifunze Kiswahili -3
da kuomba radhi kwa wasomaji wapya wa gazeti hili kuwa baadhi ya maelezo nitakayotoa pengine ni marudio ya maelezo ya hapo awali lakini yatawasaidia wengine. Kwa hiyo makala yangu ya leo yana lengo ya kile nilichowahi kuandika hapo awali kwa kuyakosoa magazeti ya Kiswahili. Baada ya kuyachunguza nimegundua kuwa yako makosa yaliyojitokeza ambayo yanatokana na uzembe wa waandishi wa kutofanya utafiti wa kutosha kwa mada husika ambapo makosa mengine yanatokana na udhaifu katika ujuzi wa misingi...
9 years ago
Mwananchi17 Sep
Jifunze Kiswahili -2-
di kisichopungua miaka miwili, nimekuwa nikipitia magazeti ya Kiswahili yanayochapishwa hapa nchini. Nimegundua kuwa baadhi ya waandishi na wahariri hawako makini katika matumizi ya Kiswahili fasaha. Pamoja na juhudi zangu za kusahihisha makosa yanayojitokeza katika magazeti, bado juhudi zangu hazijazaa matunda ya kuridhisha.
9 years ago
Mwananchi13 Oct
Jifunze Kiswahili 2
Kabla ya kuanza makala yangu, napenda kuwafahamisha wasomaji wangu kuwa baadhi yao wameniletea  maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali ya msingi katika lugha. Ni jambo jema kama nitawaleteeni  mawazo hayo ili nanyi muweze kuyatafakari. Kwa mfano mwandishi mmoja mwenye simu na. 0713 614058 aliniandikia, akisema, “ Ndugu, Mtanzania huyu asiyejiamini katika biashara za kimataifa kwa sababu...
9 years ago
Mwananchi23 Oct
Jifunze Kiswahili Sanifu
Katika makala zangu zilizotangulia, nilijikita zaidi katika makosa yanayojitokeza katika magazeti ya Kiswahili ya kila siku. Wanaosoma makala haya baadhi wamefanikiwa kuepuka makosa yao. Ni matumaini yangu kuwa moyo wa kupenda kujiendeleza uendelee kuimarika na kushamiri kwa lengo la kuwa mfano wa kuigwa kwa waandishi wengine.
10 years ago
Mwananchi16 Jun
Jifunze Kiswahili na uwafunze wengine 4
MAKOSA yanayojitokeza katika magazeti mengi ya Kiswahili yatokana na waandishi kutokuwa makini na wengine kukosa ujuzi wa kutosha katika sarufi na fasihi ya Kiswahili. Kwa kuwa makosa haya yanaendelea kujitokeza, makala zangu zina nia ya kupunguza makosa hayo kwa kunukuu sentensi chache kwenye magazeti na kurekebisha makosa pamoja na kutoa maelekezo. Nimeweza kunukuu sentensi chache lakini kwa uchunguzi wa kina yako makosa mengi sana ya upatanishi wa kisarufi, matumizi mabaya ya...
Top 10
Tanzania Today
Today Breaking News,Tanzania World News
13-February-2025 in Tanzania