Mahakama ya Kadhi, ripoti ya Msolla kutikisa Bunge
BUNGE linaendelea na mkutano wake wa 18, ambao kamati mbalimbali zitaendelea kuwasilisha taarifa kwa ajili ya majadiliano. Licha ya kamati za kisekta na zisizo za kisekta, kabla ya Bunge kuahirishwa wiki hii, pia Kamati Teule iliyoundwa kuchunguza na kuchambua Sera mbalimbali zinazohusu masuala ya ardhi, kilimo, mifugo, maji na uwekezaji kubaini kasoro zilizomo katika matumizi ya ardhi, pia itawasilisha taarifa yake.
habarileo
Habari Zinazoendana
10 years ago
Mtanzania12 Sep
Mjadala Mahakama ya Kadhi wazidi kutikisa Bunge
![Bunge](http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2014/08/Bunge.jpg)
Bunge
NA WAANDISHI WETU, DODOMA
MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, Abdallah Mtutura (CCM), amewataka wajumbe wa Bunge hilo ambao ni Waislamu, washirikiane kuipinga Rasimu ya Katiba kama Mahakama ya Kadhi haitaruhusiwa katika Katiba mpya.
Akichangia sura za nne na 10 za Rasimu ya Katiba bungeni mjini hapa juzi, Mtutura alisema kitendo cha baadhi ya wajumbe kuonyesha dalili za kuipinga mahakama hiyo, hakiwezi kukubalika kwa kuwa ni muhimu kwa Waislamu wanaoiamini.
“Mheshimiwa Makamu...
10 years ago
Mwananchi28 Jan
Wabunge wawe wamoja mijadala kuhusu Ripoti ya CAG, Mahakama ya Kadhi
10 years ago
Mtanzania05 Sep
Mahakama ya Kadhi yazikwa
![Samia Hassan Suluhu](http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2014/06/Samia-Hassan-Suluhu.jpg)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan
Rachel Mrisho, Dodoma
SUALA la Mahakama ya Kadhi ambalo lilizua mjadala mkali kwenye Kamati za Bunge la Bunge Maalumu la Katiba na kuundiwa kamati ndogo iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hasan, limezikwa rasmi.
Hali hiyo imejidhihirisha jana kutokana na kutozungumziwa katika uwasilishaji wa maoni ya walio wengi, wakati kamati hizo zikiwasilisha maoni yake juu ya sura ya tisa na 10.
Imedaiwa...
10 years ago
Mwananchi19 Jan
Mahakama ya Kadhi Utata
10 years ago
Habarileo28 Aug
Mahakama ya Kadhi yawekwa kiporo
SUALA la Mahakama ya Kadhi limeleta mjadala mkali katika majadiliano na wabunge wameamua suala hilo lisiingizwe kwenye Katiba. Mjadala huo mkali uliibuka katika Kamati namba Saba ilipojadili sura ya Nne ya kwenye rasimu hiyo inayozungumzia juu ya uhuru wa imani ya dini ambapo Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hassan Ngwilizi alisema baada ya mjadala mkali wamekubaliana kutoingizwa kwenye Katiba.
10 years ago
Habarileo08 Feb
Mahakama ya Kadhi yasogezwa mbele
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameeleza sababu za Bunge kushindwa kujadili miswada kadhaa, ikiwemo uliohusu Marekebisho ya Sheria ya Kiislamu, inayotambua Mahakama ya Kadhi.
10 years ago
Habarileo10 Sep
Mahakama ya Kadhi yawagawa wabunge
MAHAKAMA ya Kadhi imetikisa mjadala wa Bunge Maalumu la Katiba jana. Hali hiyo inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya wajumbe ambao walipata fursa ya kuchangia waliendelea kuwashawishi wenzao wakubali mahakama hiyo iingizwe kwenye Katiba kwani ni chombo muhimu kwa waumini wa dini ya Kiislamu.
10 years ago
Habarileo29 Mar
JK aweka msimamo Mahakama ya Kadhi
RAIS Jakaya Kikwete amefafanua msimamo wa Serikali katika mjadala unaoendelea wa Mahakama ya Kadhi, na kuweka wazi kuwa Serikali haina mpango wa kuianzisha, wala kuiendesha.
10 years ago
Mwananchi30 Sep
Pinda aiokoa Mahakama ya Kadhi