Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Walemavu kufaidika na huduma za NHIF

MAKUNDI mbalimbali ya wajasiriamali wa jamii ya wenye ulemavu yataanza kunufaika na huduma zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), imefahamika jijini hapa. Mkurugenzi wa huduma za mfuko wa afya ya jamii kutoka NHIF, Rehani Athumani, aliyasema hayo alipokuwa akitoa salamu za NHIF wakati wa uzinduzi wa tawi la Vicoba kwa watu wenye ulemavu katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya Benjamin Mkapa. Awali, Rais wa Vicoba Tanzania, Devota Likokola (MB), aliushukuru Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kushirikiana na wana-Vicoba katika utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu huduma zake na kuuhimiza kuharakisha zoezi la utoaji elimu kwa watu wenye ulemavu ili hatimaye waweze kunufaika na huduma za matibabu. Aidha, Likokola alimshukuru Dk Reginald Mengi ambaye ni mdhamini wa jamii ya watu wenye ulemavu na Benki ya Posta kwa kuunga mkono jamii ya walemavu kujikwamua kiuchumi wakati wote. Katika risala yao mbele ya mdhamini wao, Ramadhani Madabida ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, walisema kukosa maeneo ya kufanyia biashara na mitaji ni baadhi ya changamoto zinazowakabili katika mapambano yao ya kujikomboa kiuchumi. Madabida aliahidi kuipatia ufumbuzi changamoto ya maeneo ya kufanyia biashara kwa kushirikiana na Meya wa Manispaa ya Kinondoni kama hatua ya awali na pia aliahidi kuwachangia kiasi cha milioni moja kuongezea mtaji wao.MAKUNDI mbalimbali ya wajasiriamali wa jamii ya wenye ulemavu yataanza kunufaika na huduma zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), imefahamika jijini hapa.

habarileo

Read more


Habari Zinazoendana

10 years ago

Michuzi

WATOA HUDUMA MKOANI LINDI WAASWA KUCHANGAMKIA MIKOPO INAYOTOLEWA NA NHIF ILI KUBORESHA HUDUMA ZA MATIBABU

Kaimu katibu tawala wa Mkoa wa Lindi Grayson Mwaigombe amewataka waganga wakuu wa hospitali kuanzia ya mkoa na wilaya,kuchangamkia mikopo ya riba nafuu inayotolewa na NHIF,ili waweze kuboresha huduma na pia kuwa chanzo kingine cha mapato ya hospitali,kwani wananchi kwa sasa wanahitaji huduma bora na stahiki,aliyesema hayo wakati wa elimu ya uhamasishaji watoa huduma wa Serikali, mashirika ya dini na watu binafsi waliosajiliwa na mfuko,kuchangamkia fursa ya mikopo ya vifaa tiba,ukarabati wa...

 

9 years ago

Habarileo

NHIF yatangaza maboresho ya huduma

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umetangaza kuboresha orodha ya huduma na gharama zinazolipwa kwa watoa huduma kwa ajili ya kufanikisha huduma hizo. Aidha, imefunga mfumo wa malipo wa elektroniki katika maduka yote ya dawa yaliyosajiliwa na NHIF ambao unaruhusu uchakataji wa madai ya dawa kwa kila siku.

 

10 years ago

Tanzania Daima

Wastaafu wafurahia huduma za NHIF

BAADHI ya walimu wastaafu wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, wameupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuwa na fao la wastaafu linalowapa uhakika wa matibabu...

 

11 years ago

Habarileo

Watoa huduma NHIF kukopeshwa bililioni 10/-

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Hamis MdeeBODI ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), imeidhinisha Sh bilioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha watoa huduma ili waweze kupata vifaa tiba na kukarabati maeneo yao ya kutolea huduma.

 

10 years ago

Michuzi

NHIF kuendelea kuboresha huduma za afya nchini.




Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Raphael Mwamoto akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)kuhusu mpango wa kuendelea kuboresha huduma za Afya nchini, wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Uwekezaji kutoka Mfuko huo Bw. Deusdedit Rutazaa.
Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Uwekezaji kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Deusdedit Rutazaa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)...

 

11 years ago

Michuzi

NHIF na huduma bora Wiki ya Utumishi wa Umma

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Hamis Mdee akitoa maelekezo kwa Maofisa wa Mfuko huo katika maonesho ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja. Maofisa wa Mfuko katika banda la NHIF kitengo cha Usajili wa wanachama wakiendelea na uhakiki wa nyaraka kwa ajili ya vitambulisho. Wadau waliotembelea banda la NHIF wakipatiwa huduma. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Hamis Mdee akitaka ufafanuzi wa jambo katika banda la Mamlaka ya...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani