Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Rais amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu RAHCO

Rais John Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hodhi ya rasilimali za Reli Tanzania RAHCO Mhandisi Benhadard Tito kupisha uchunguzi wa kina kutokana na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi uliobainika katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.

 Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema Rais Magufuli amefikia uamuzi huo baada ya kuitisha kikao cha wataalamu kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali...

StarTV

Read more


Habari Zinazoendana

9 years ago

Dewji Blog

Rais amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa RAHCO

IMG_7092

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kuhudumia Miundombinu ya Reli (RAHCO) Benhadard Tito (katikati). (Picha na Maktaba).

Rais wa Jamhuri ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) Mhandisi Benhadard Tito ili kupisha uchunguzi wa kina kufuatia ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi uliobainika katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya...

 

9 years ago

Global Publishers

Rais Magufuli amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya RAHCO

DSC_0792Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) Mhandisi Benhadard Tito (kulia).

Rais wa Jamhuri ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) Mhandisi Benhadard Tito ili kupisha uchunguzi wa kina kufuatia ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi uliobainika katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Katibu...

 

10 years ago

Mwananchi

Sitta amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu TPA, alalamikiwa kwa ubabaishaji

Waziri wa Uchukuzi Samuel Sitta amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande baada ya kuwepo malalamiko ya ubabaishaji katika zabuni mbalimbali za mamlaka hiyo.

 

9 years ago

Michuzi

BREAKING NYUZZZZZZ......: RAIS MAGUFULI AMSIMAMISHA KAZI KAMISHNA MKUU WA TRA

Raisi wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania, Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli amemsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 27 Nov. 2015, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Rished Bade kufuatia ziara ya kushtukiza ya Waziri Mkuu, Mh. Majaliwa Kasimu Majaliwa mapema leo asubuhi Bandarini jijini Dar es salaam.
Hatua hiyo imekuja baada kubaini kupitishwa kwa makontena zaidi ya 300 na kusababishia hasara Serikali ya zaidi ya shilingi bilioni 80.
Rais Magufuli pia amemteua  Katibu...

 

10 years ago

Vijimambo

SITTA AMSIMAMISHA KAZI KAIMU MKURUGENZI WA TPA MADENI KIPANDE

Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta (pichani kulia akizungumza na wanahabari leo bandarini) amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Eng Madeni Shamte Kipande kwa tuhuma za utendaji mbovu, ikiwa ni pamoja na kutokuwepo kwa uwazi kwenye mamlaka hiyo hususani katika michakato ya zabuni mbalimbali zinazotangazwa na mamlaka hiyo.
Pamoja na kuchukua uamuzi huo Mhe. Sitta, ameunda tume ya watu sita itakayokuwa na jukumu la kuchunguza tuhuma zinazomkabilia...

 

9 years ago

Dewji Blog

Waziri Ummy Mwalimu amsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Ocean Road

Ocean Road Cancer Institute, acting chief executive officer, Diwani Msemo speaks at press conference in Dar es Salaam yesterday. 44,000 Tanzanians are diagnosed with cancer disease every year but only 8800 stands a good chance of being full cured. PHOTO| SALIM SHAO

Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo.

 

9 years ago

Michuzi

WAZIRI WA AFYA AMSIMAMISHA KAZI KAIMU MKURUGENZI WA TAASISI YA OCEAN ROAD DK.DIWAN MSEMO.


Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
Na Chalila Kibuda,Globu ya JamiiWAZIRI wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk.Diwani Msemo ili kupisha uchunguzi pamoja na mambo mengine ili kubaini  mgongano wa kimaslahi ulioathiri utendaji wa taasisi  hiyo chini ya kaimu mkurugenzi huyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya...

 

9 years ago

Mwananchi

Mkuu wa mkoa amsimamisha kazi mhandisi wa wilaya

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Fatma Mwassa ameagiza kusimamishwa kazi Mhandisi wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Suleiman Paul na Ofisa Ugavi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Denis Nyisaba ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuisabababishia Serikali hasara ya mamilioni ya fedha.

 

10 years ago

Dewji Blog

Katibu Mkuu Kiongozi amsimamisha kazi ndugu Maswi kupisha uchunguzi!

DSC_0453

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, amemsimamisha kazi kwa muda Ndugu Eliakim Maswi (pichani),  Katibu Mkuu ya Wizara ya Nishati na Madini, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake, kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

Balozi Sefue amemsimamisha kazi Ndugu Maswi kuanzia leo, Jumanne, Desemba 23, 2014, kwa kutumia madaraka aliyonayo kama Mamlaka ya Nidhamu kwa Watumishi wa Umma wanaoteuliwa na Rais, wakiwemo...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani