Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Brigedia Jenerali Mbita afariki dunia

mbitaJonas Mushi na Patricia Kimelemeta, Dar es Salaam

MMOJA wa Watanzania waliofanikisha ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika,Brigedia Jenerali Hashim Mbita (82), alifariki dunia jana katika Hospitali Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo ambako alikuwa amelazwa kwa muda mrefu.

Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwa marehemu Chang’ombe Madukani Dar es Salaam jana, mtoto wa marehemu Iddi Mbita alisema baba yake alifariki dunia saa 3:30 asubuhi baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu...

Mtanzania

Read more


Habari Zinazoendana

10 years ago

Michuzi

JUST IN: gwiji la ukombozi wa afrika kusini brigedia jenerali hashim mbita afariki dunia leo dar es salam


Habari zilizotujia hivi punde zinasema Brigedia Jeneral Mstaafu Hashim Mbita aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Kamati ya Ukombozi ya uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), amefariki dunia asubuhi hii katika hospitali kuu ya jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam. 
Mzee Mbita atakumbukwa Tanzania,  bara zima la Afrika na dunia kwa jumla kama kamanda mahiri aliyeshiriki kikamilifu katika uondoshaji wa utawala wa ukoloni  barani Afrika, hususan utawala kidhalimu wa makaburu  Zimbabwe na  Afrika...

 

10 years ago

Dewji Blog

Tanzania yampoteza mtu muhimu, ni Brigedia Jenerali Mstaafu Hashim Mbita aliyefariki dunia mapema leo

Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Hashim Mbita

Taifa likiwa katika maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano wa Tanzania Bar na Zanzibar, mapema leo limepata pigo baada ya kuondokewa na mtu muhimu na aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamati ya Ukombozi ya uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Brigedia Jenerali Mstaafu Hashim Mbita aliyefariki katika dunia majira ya asubuhi katika hospitali kuu ya Jeshi, Lugalo,  jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa duru za habari kutoka familia ya...

 

10 years ago

Michuzi

BRIGEDIA JENERALI MSAAFU HASHIMU SAID MTEZO AFARIKI DUNIA

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (TWTZ) linasikitika kutangaza kifo cha Brigedia Jenerali  (mstaafu) Hashimu Said Mtezo kilichotokea tarehe 04 Oct 14 kwa ugonjwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo     Dar es Salaam alipokuwa akipata matibabu.              

Alizaliwa Machi 18, 1945 Wilaya ya Dodoma mjini katika Mkoa wa Dodoma, alisoma katika shule ya Sekondari ya Tabora kuanzia mwaka 1962 hadi alipohitimu Kidato cha Sita mwaka 1967.  Alijiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania tarehe...

 

5 years ago

Bongo5

Tanzia: Brigedia Jenerali (mstaafu) Albert Costantino Frisch afariki dunia

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linasikitika kutangaza kifo cha Brigedia Jenerali Albert Costantino Frisch (mstaafu) kilichotokea tarehe 13 Aprili 2017.

Marehemu Brigedia Jenerali Albert Costantino Frisch (mstaafu) alizaliwa tarehe 13 Novemba 1944, mtaa wa Uhuru, Tarafa ya Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam. Alisoma na kuhitimu Shule ya Msingi mkoani Dar es Salaam na baadaye kuendelea na masomo ya Sekondari katika Shule ya Sekondari St. Joseph Convert School,...

 

10 years ago

Mtanzania

Nchi 16 wamzika Brigedia Jenerali Mbita

Na Patricia Kimelemeta, Dar es Salaam

VIONGOZI wa nchi mbalimbali za Afrika jana walijitokeza kuaga mwili wa aliyekua katibu mtendaji wa kamati ya ukombozi kusini Afrika, Brigedia Jenerali Hashim Mbita katika Hosipitali ya jeshi ya Lugalo, Dar es salaam.

Mbali na nchi hizo, Rais Jakaya Kikwete aliongoza kuaga mwili wa marehemu Mbita akifuatana na Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda pamoja na viongozi waandamizi wa jeshi na vyama vya siasa.
Mwili wa Mbita uliagwa jana...

 

10 years ago

GPL

HATIMAYE BRIGEDIA JENERALI MBITA AZIKWA

Mwili wa Brigedia Jenerali Hashim Mbita ukiswaliwa Msikitini. Mwili wa Marehemu Mbita ukiingizwa kwenye gari maalum la Jeshi kwa ajili ya kupelekwa makaburi ya Kisutu Dar kwa maziko.…

 

10 years ago

Mtanzania

Brigedia Jenerali Mbita kuzikwa leo

mbitaAdam Mkwepu na Easther Mnyika, Dar es Salaam
ALIYEKUWA Katibu Mtendaji wa Kamati ya Ukombozi ya uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Brigedia Jenerali mstaafu Hashim Mbita (82), anatarajiwa kuzikwa leo jijini Dar es Salaam.
Mbita aliyefariki dunia Mei 26, mwaka huu katika Hospitali ya Jeshi Lugalo, anatarajiwa kuzikwa leo alasiri katika makaburi ya Kisutu.
Kifo cha mpigania uhuru huyo wa nchi za Afrika kimewagusa viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali ambapo Katibu Mkuu wa Chama...

 

10 years ago

Mwananchi

JK aongoza mamia kumzika Brigedia Jenerali Mbita

Dar es Salaam. Mamia ya waombolezaji wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete jana walijitokeza katika Makaburi ya Kisutu jijini hapa kuuzika mwili wa Brigedia Jenerali Hashim Mbita aliyefariki dunia mwanzoni mwa wiki hii.

 

10 years ago

Vijimambo

BRIGEDIA JENERALI ( MSTAAFU ) HASHIM MBITA AZIKWA MAKABURI YA KISUTU, JIJINI DAR

Viongozi mbali mbali wa Dini ya Kiislam wakishiriki pamoja na waumini wao kwenye Ibada ya kuuswalia mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali(Mstaafu) Hashim Mbita kwenye Msikiti wa Mtoro, Kariakoo na baadae kwenda kuuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele, Makaburi ya Kisutu, Jijini Dar es Salaam. Picha zote na Hamis Makuka.Maelfu ya waunini wa kiislam wakishiriki kuubeba mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali(Mstaafu) Hashim Mbita wakati wakiutoa kwenye Msikiti wa Mtoro, Kariakoo na tayari kwa kwenda...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani