Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Hatma ya kesi ya meta 200 kutolewa leo

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo itatoa uamuzi kuhusu shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbunge wa Viti Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Amy Kibatala likihoji uhalali wa wapigakura kukaa mita 200 kutoka kwenye vituo vya kupigia kura.

habarileo

Read more


Habari Zinazoendana

10 years ago

Habarileo

Mahakama Kuu yaombwa kutupa ‘kesi ya meta 200’

MW A N A S H E R I A Mkuu wa Serikali (AG) ameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kutupilia mbali kesi ya kikatiba kuhusu haki ya wananchi kukaa meta 200 kutoka katika kituo cha kupigia kura. Kesi hiyo ilianza kusikilizwa jana mbele ya jopo la majaji Sakieti Kihiyo, Aloysius Mujulizi na Lugano Mwandambo.

 

10 years ago

StarTV

 Uamuzi kesi wa mita 200  iliyofunguliwa kutolewa Oktoba 23

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam imetoa maelekezo  kuwa Oktoba 23 mwaka huu itatoa Uamuzi dhidi ya Kesi iliyofunguliwa ya Kikatiba kuhusu Tafsiri sahihi ya Umbali anaotakiwa kusimama Mpiga kura baada ya kupiga kura.

Kesi hiyo Namba 37 ya Mwaka 2015 iliyofunguliwa na Amy Kibatala anayeongozwa na Wakili Peter Kibatala, ambaye anataka Tafsiri ya kifungu 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kuhusu kukaa umbali wa mita mia 200 baada ya kupiga kura

 Kesi hiyo imeanza kuunguruma mapema Wiki...

 

10 years ago

Mtanzania

Uamuzi mita 200 kutolewa leo

mtz4NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM

JOPO la majaji watatu wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo watatoa uamuzi wa mvutano mkali kuhusu kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.

Mwenyekiti wa jopo hilo, Sekieti Kihiyo, alisema hayo jana akiwa pamoja na majaji wenzake, Aloycius Mujuluzi na Lugano Mwandambo.

“Jana (juzi) tuliwaambia leo tutatoa maelekezo muhimu, kesho(leo) saa nne tutatoa uamuzi,”alisema Jaji
Kihiyo.

Majaji hao walifikia hatua ya kutoa uamuzi huo baada ya kusikiliza hoja...

 

11 years ago

StarTV

Hatma Kesi ya Pistorious ni leo.

Leo Jaji Tokozile Masipa ataanza kusoma maelezo ya mwisho ya kesi ya Oscar Pestorius yatakayachukua siku nne.

 
Akipitia maelezo ya upande wa mashitaka na upande wa utetezi katika kesi hii ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini.

 
Aliepatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake bila kukusudia .

 
Mengi yamesemwa na raia wa A-Kusini katika kesi hii kwamba Jaji hakuonesha uadilifu kumpata Oscar Pestorius na hatia ya kuua bila kukusudia badala ya kuua kwa makusudi.

 

BBC

 

9 years ago

Mtanzania

Kesi ya Mawazo kutolewa hukumu leo

Alphonce  MawazoNA BENJAMIN MASESE, MWANZA

JAJI wa Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Lameck Mlacha, anatarajia kutoa hukumu juu ya mvutano wa kuuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Geita marehemu Alphonce Mawazo jijini Mwanza.

Jaji Mlacha anatarajia kutoa hukumu hiyo leo saa saba mchana baada ya pande zote mbili kueleza hoja zao.

Mawakili wa Serikali, Seth Mkemwa na Emilly Kilia ambao wanamtetea Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mwanza, Charles Mkumbo aliyezuia...

 

10 years ago

Habarileo

Mahakama Kuu yazuia kulinda kura meta 200

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imepiga marufuku mtu yeyote asikusanyike wala kukaa umbali wa meta 200 kutoka katika kituo cha kupiga kura siku ya kesho, wakati wananchi wakipiga kura.

 

9 years ago

Mwananchi

Uamuzi gharama za kesi ya ubunge Mbagala kutolewa leo

Mahakama Kuu leo inatarajiwa kutoa uamzui wa maombi ya tathmini ya gharama za usikilizwaji wa kesi ya ubunge katika kesi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 wa Jimbo la Mbagala, jijini Dar es Salaam.

 

10 years ago

Habarileo

Kesi ya kukaa mita 200 leo

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana imeshindwa kusikiliza kesi kikatiba kuhusu uhalali wa kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura, kwa kuwa upande wa Jamhuri haujawasilisha utetezi wao.

 

10 years ago

Mtanzania

Kesi ya mita 200 kuanza leo

Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam

JOPO la majaji watatu wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo linatarajia kuanza kusikiliza kesi ya kikatiba kuhusu haki ya mpigakura kukaa umbali wa mita 200 kama ni sahihi au la.

Jopo hilo la majaji Seleman Kihiyo, Aliyisius Mujuluzi na Lugano Mwandambo, liliteuliwa baada ya mgombea ubunge wa Viti Maalumu Jimbo la Kilombero kupitia Chadema, Amy Kibatala, kufungua kesi hiyo kupitia kwa wakili Peter Kibatala.

Katika maombi yake, anaomba Mahakama Kuu ya...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani