Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


KITUO CHA POLISI BUNJU CHACHOMWA MOTO

Baadhi ya wakazi wa Bunju wamevamia na kukichoma moto kituo cha polisi Bunju A baada ya polisi kufyatua mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya wananchi waliofunga barabara baada ya mwanafunzi mmjoa kugongwa na gari na kufariki.Polisi walilazimika kukimbia na gari lao baada ya kuona wananchi wanawazidi nguvu kwa kurusha mawe na kukiacha kituo hicho bila ya ulinzi ndipo wananchi walipokivamia kituo kuvunja milango na kuwatoa wahalifu waliokuwa wakishikiliwa na kisha kukichoma moto

Vijimambo

Read more


Habari Zinazoendana

10 years ago

Michuzi

NEWZZ ALERT:KITUO CHA POLISI BUNJU CHACHOMWA MOTO.

Baadhi ya Polisi wakiwatawanya watu (hawapo pichani) kwa mabomu ya machozi mara baada ya tukio la kuchomwa moto kituo cha polisi Bunju, tukio hilo limetokea.Kituo cha polisi Bunju kilichopo nje kidogo ya jiji la Dar kimechomwa moto na baadhi ya Wananchi kufuatia tukio la kudaiwa kwa Mwanafunzi mmoja kugongwa na gari na kufa papo hapo Sehemu ya kituo hicho cha Polisi Bunju kikiteketea kwa moto mara baada ya kuchomwa moto na wananchi kufuatia tukio la kudaiwa kwa Mwanafunzi mmoja kugongwa na...

 

10 years ago

Habarileo

Bunju wateketeza kituo cha Polisi

WANANCHI wa Bunju jijini Dar es Salaam wamechoma moto kituo cha polisi cha Bunju A na gari lililodaiwa kusababisha ajali ya mwanafunzi na kusababisha kifo.

 

10 years ago

GPL

WANANCHI BUNJU WACHOMA KITUO CHA POLISI

Kituo cha Polisi Bunju B kikiteketea baada ya kuchomwa na wananchi wenye hasira kali. Moshi mkubwa kutoka eneo hilo la kituo. Baadhi ya wakazi wa Bunju leo wamevamia na kukichoma moto Kituo cha Polisi Bunju A baada ya polisi kufyatua mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya wananchi waliofunga barabara baada ya mwanafunzi wa darasa la nne Shule ya Msingi ya Bunju A kugongwa gari na kufariki leo asubuhi. Polisi… ...

 

11 years ago

Mwananchi

Raia wawili, askari wauawa Moro, kituo chachomwa moto

Watu watatu, akiwamo askari polisi wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya kuzuka mapambano kati ya polisi na raia katika Kijiji cha Igwati, Tarafa ya Malinyi Wilaya ya Ulanga, Morogoro.

 

9 years ago

Mtanzania

Kituo cha Redio chachomwa Z’bar

20151203044410-8Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

WATU wasiojulikana wakiwa na silaha wamevamia studio za kituo cha Radio Hits FM kilichopo eneo la Migombani mjini Unguja na kukichoma moto kwa kutumia mafuta yanayosadikiwa kuwa ni petroli.

Akizungumza jana mjini Unguja, msemaji wa kituo hicho, Juma Ayoub Amohamed, alisema tukio hilo lilitokea saa 7:30 usiku wa kuamkia jana ambapo zaidi ya watu 15 walivamia studio hiyo na kufanikiwa kuchoma moto.

Alisema hadi sasa bado hawajajua nini chanzo cha kufanyiwa hivyo, na...

 

5 years ago

BBCSwahili

Mauaji ya George Floyd: Waandamanaji wakichoma moto kituo cha polisi cha Minneapolis, Marekani

Marekani yashuhudia usiku wa tatu wa maandamano kutokana na kifo cha mwanaume mweusi

 

10 years ago

GPL

HIVI NDIVYO KITUO CHA POLISI KILIVYOCHOMWA MOTO!

Na Waandishi Wetu TUKIO la wananchi kuchoma Kituo Kidogo cha Polisi cha Bunju A kilichopo wilayani Kinondoni, jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita lilizua mshtuko wa aina yake na kuweka rekodi mbaya nchini, Uwazi linakupa habari kamili. Soma zaidi hapa ===>http://bit.ly/1GiCgZo

 

10 years ago

Mwananchi

Mwanafunzi agongwa, wakazi wachoma moto kituo cha polisi

Dar es Salaam. Wakazi wa Bunju ‘A’, wamechoma kituo cha polisi cha eneo hilo kwa kile kilichodaiwa kushindwa kuelewana na askari baada ya mwanafunzi wa darasa la nne kugongwa na gari na kufariki dunia.

 

11 years ago

Michuzi

BREAKING NEWS;KITUO CHA POLISI MOSHI KINAWAKA MOTO

TAARIFA ZA UHAKIKA ZILIZOTUFIKIA KATIKA CHUMBA CHA HABARI YA GLOBU YA JAMII HIVI PUNDE,ZINAELEZA KUWA KITUO CHA POLISI MOSHI MKOANI KILIMANJARO KINAWAKA MOTO,AIDHA MPAKA SASA CHANZO CHA MOTO HUO BADO HAKIJAJULIKANA.
HABARI ZAIDI TUTAZIDI  KUWALETEA KADIRI YA ZITAKAVYOKUWA ZIKIINGIA.

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani