Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Mvua yaua watu, nyumba zasombwa

MVUA iliyonyesha juzi na jana, ikiambatana na upepo mkali katika mikoa mbalimbali nchini, imeleta madhara na kusababisha vifo vya watu kadhaa. Jijini Dar es Salaam, nyumba nyingi zimebomolewa na kuzingirwa na maji, na miundombinu imekatika, ikiwemo kufunikwa kwa madaraja muhimu na adha za kila aina.

habarileo

Read more


Habari Zinazoendana

11 years ago

Mwananchi

Mvua yaua, yaezua nyumba 62

Nyumba 62 zilizopo katika Vijiji vya Wilaya ya Kilindi, zimeezuliwa na nyingine kubomoka kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali kunyesha kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tanga.

 

11 years ago

Habarileo

Mvua yaua mmoja, yaezua nyumba 85

MVUA zimeleta maafa mkoani Kilimanjaro baada ya mtu mmoja kufariki dunia sanjari na nyumba zaidi ya 85 kuezuliwa mapaa. Mkuu wa Wilaya ya Hai, Novatus Makunga, alisema kaya takribani 85 zimekosa makazi. Aidha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kibohehe, na Shule ya Msingi Kishare wamekosa pa kusomea kutokana na baadhi ya madarasa kuezuliwa mapaa kwa upepo.

 

10 years ago

Habarileo

Mvua yaua watu 38 Kahama

Wakazi wa Kahama mkoani Shinyanga wakipita kwenye eneo lililofurika maji kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo iliyonyesha mkoani humo juzi.MAAFA makubwa yameikumba Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga baada ya watu 38 kufa papo hapo na wengine 82 kujeruhiwa, kutokana na mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo mkali, iliyonyesha katika Kijiji cha Mwakata Kata ya Isaka.

 

10 years ago

Mwananchi

Mvua ya mawe yaua watu 42 Kahama, 91 wajeruhiwa

Mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha juzi usiku imesababisha maafa katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambako zaidi ya watu 42 wameuawa, wakiwamo saba wa familia moja na wengine 91 kujeruhiwa vibaya.

 

9 years ago

Mwananchi

Mvua yaua watu watatu, kaya zaidi ya 70 zakosa makazi

Watu watatu wamefariki dunia na familia zaidi ya 70 zimekosa mahala pa kuishi, huku mifugo zaidi ya 150 ikisadikiwa kufa baada ya kukumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani Arumeru mkoani Arusha.     

 

11 years ago

Tanzania Daima

Mvua yaua watano Singida

MVUA kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia juzi mkoani Singida, imesababisha vifo vya watu watano, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji wakati wakivuka mto Nalala wilayani Iramba. Kamanda wa...

 

10 years ago

Habarileo

Mvua kubwa yaua Dar

Wakazi wa Dar es Salaam wakipita ndani ya dimbwi la maji ya mvua yaliyotuama katika Barabara ya Bibi Titi jirani na kituo cha daladala ya chumba cha Dada Pendo, cha Akiba kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jana. (Picha na Mroki Mroki).MVUA iliyonyesha jijini Dar es Salaam jana, imeleta balaa baada ya kuua watu wawili, katika maeneo tofauti ya jiji, likiwemo tukio la mtoto wa miaka minane kufa baada ya kuzidiwa na maji yaliyoingia ndani ya nyumba aliyokuwa amelala.

 

10 years ago

Habarileo

Mvua yaua 5 Dar es Salaam, yajeruhi

Nyumba za wakazi wa Bonde la Hananasif, Kinondoni zikiwa zimefunikwa na maji baada ya bonde hilo kufurika maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Fadhili Akida).HALI ni tete katika jiji la Dar es Salaam, kutokana na mvua ya masika iliyonyeshwa kwa siku tatu na kusababisha vifo vya watu watano, huku nyumba nyingi zikiwa zimezingirwa na maji.

 

10 years ago

Mtanzania

Mvua yaua sita Mwanza, Kagera

Baadhi ya wakazi wa Mwanza wakiangalia nyumba iliyoporomokewa na mwamba katika Mtaa wa Nyerere A Sinai-Mabatini jana.

Baadhi ya wakazi wa Mwanza wakiangalia nyumba iliyoporomokewa na mwamba katika Mtaa wa Nyerere A Sinai-Mabatini jana.

SITTA TUMMA NA RENATHA KIPAKA

WATU sita wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa katika matukio mawili tofauti yaliyoambatana na mvua katika mikoa ya Mwanza na Kagera.

Katika tukio la jijini Mwanza, vilio na simanzi jana vilitawala kwa wakazi wa maeneo ya Sinai-Mabatini, baada ya vifo vya watu wanne wa familia mbili tofauti, vilivyotokana na mvua iliyosababisha miamba...

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani