Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Wabunge wavurugana Mahakama ya Kadhi

Waziri Mkuu, Mizengo PindaBAADA ya kutokea kutoelewana miongoni mwa wabunge juu ya marekebisho ya muswada wa sheria inayoruhusu kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kuna haja ya Serikali kutafakari upya kuhusu suala hilo kabla ya kuliwasilisha bungeni.

habarileo

Read more


Habari Zinazoendana

10 years ago

Mtanzania

Mahakama ya Kadhi yawavuruga wabunge

Na Debora Sanja na Fredy Azzah, Dodoma
WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana nusura wazichape kavukavu baada ya kutofautiana juu ya uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi.
Hali hiyo ilijitokeza wakati wabunge hao wakiwa katika semina iliyohusu Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali, ambapo miongoni mwa sheria zilizomo ndani yake ni pamoja na ile ya Mahakama ya Kadhi.
Sakati hilo lilitokea katika semina kuhusu muswada huo unaotarajiwa kuwasilishwa bungeni keshokutwa...

 

10 years ago

Habarileo

Mahakama ya Kadhi yawagawa wabunge

MAHAKAMA ya Kadhi imetikisa mjadala wa Bunge Maalumu la Katiba jana. Hali hiyo inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya wajumbe ambao walipata fursa ya kuchangia waliendelea kuwashawishi wenzao wakubali mahakama hiyo iingizwe kwenye Katiba kwani ni chombo muhimu kwa waumini wa dini ya Kiislamu.

 

10 years ago

Mwananchi

Wabunge wawe wamoja mijadala kuhusu Ripoti ya CAG, Mahakama ya Kadhi

Bunge jana lilianza mkutano wake wa 18 mjini Dodoma likiwa na masuala mengi mazito katika ajenda yanayopaswa kujadiliwa katika muda mfupi tu wa wiki mbili. Hicho ni kikao chake cha kwanza mwaka huu, ambacho kinakuja baada ya mkutano wake wa 16/17 uliofanyika Novemba mwaka jana na kugubikwa na mjadala mkali kuhusu uchotwaji wa fedha kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow. Baadhi ya watendaji serikalini wamefikishwa mahakamani, huku mawaziri wawili na mwanasheria mkuu wa Serikali wakijiuzulu.

 

10 years ago

Mtanzania

Mahakama ya Kadhi yazikwa

Samia Hassan Suluhu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan

Rachel Mrisho, Dodoma

SUALA la Mahakama ya Kadhi ambalo lilizua mjadala mkali kwenye Kamati za Bunge la Bunge Maalumu la Katiba na kuundiwa kamati ndogo iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hasan, limezikwa rasmi.

Hali hiyo imejidhihirisha jana kutokana na kutozungumziwa katika uwasilishaji wa maoni ya walio wengi, wakati kamati hizo zikiwasilisha maoni yake juu ya sura ya tisa na 10.

Imedaiwa...

 

10 years ago

Mwananchi

Mahakama ya Kadhi Utata

Wajumbe wa kamati tatu za Kudumu za Bunge ambazo wenyeviti wake wanatakiwa kuvuliwa nyadhifa zao kutokana na kuhusika katika kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow, ‘wanasuasua’ kuwaondoa na kuchagua viongozi wengine.

 

10 years ago

Mtanzania

Maaskofu:Mahakama ya Kadhi ya Kibaguzi

alexmalasusaJUKWAA la Wakristo Tanzania (TCF) limepinga muswada unaopendekeza kuanzishwa Mahakama ya Kadhi, likiitaka Serikali iuondoe bungeni kwa madai kuwa ni wa kibaguzi na upo kinyume na matakwa ya Katiba.
Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali ya 2014, unapendekeza pamoja na mambo mengine, marekebisho ya Sheria ya Tamko la Sheria za Kiislamu ya mwaka 1964.
Maaskofu na wajumbe wa jukwaa hilo walikutana Januari 20, mwaka huu jijini Dar es Salaam na kushauri Serikali iondoe muswada huo bungeni...

 

10 years ago

Habarileo

Mahakama ya Kadhi yawekwa kiporo

SUALA la Mahakama ya Kadhi limeleta mjadala mkali katika majadiliano na wabunge wameamua suala hilo lisiingizwe kwenye Katiba. Mjadala huo mkali uliibuka katika Kamati namba Saba ilipojadili sura ya Nne ya kwenye rasimu hiyo inayozungumzia juu ya uhuru wa imani ya dini ambapo Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hassan Ngwilizi alisema baada ya mjadala mkali wamekubaliana kutoingizwa kwenye Katiba.

 

11 years ago

Tanzania Daima

Waislamu walilia Mahakama ya Kadhi

JUMUIYA na taasisi za Kiislamu nchini zimeshangazwa kutokana na baadhi ya mapendekezo yao kutokuwamo  kwenye rasimu ya pili ya Katiba. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana,...

 

10 years ago

Habarileo

JK aweka msimamo Mahakama ya Kadhi

Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa viongozi wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Freddy Maro).RAIS Jakaya Kikwete amefafanua msimamo wa Serikali katika mjadala unaoendelea wa Mahakama ya Kadhi, na kuweka wazi kuwa Serikali haina mpango wa kuianzisha, wala kuiendesha.

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani