Jobs

Sales Representative

NORTH AMERICA ALIGN WORKERS EMPLOYMENT PROGRAM (NAAWEP)
Deadline: Oct 26, 2105




POPULAR ON YOUTUBE


Wakazi kata ya Kurasini Dar wagoma kuhama Kupisha mradi wa maegesho

Wakazi wa kata ya Kurasini Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam wamegoma kuhama katika makazi yao kupisha mradi wa ujenzi wa maegesho ya magari makubwa.

Manispaa ya Temeke imetoa amri ya kuwataka wakazi wa maeneo hayo kuhama ndani ya muda wa saa 12 kuanzia Novemba 13, vinginevyo nyumba zao zitavunjwa.

wakazi wa Kurasini jijini Dar es Salaam, wamepaza kilio chao kupinga amri ya Manispaa ya Temeke kuwataka kuhama eneo hilo kupisha ujenzi wa maegesho ya magari makubwa.

Wakizungumza na Star...

StarTV

Read more


Habari Zinazoendana

11 years ago

Tanzania Daima

Wagoma kuhama kupisha barabara

WAKAZI wa kaya 30 wa mitaa ya Majanimapana na Nguvumali zinazotarajiwa kubomolewa makazi yao kupisha ujenzi wa barabara zimetangaza mgogoro na serikali kwa kugoma kuhama na kumtaka Rais Jakaya Kikwete...

 

10 years ago

Tanzania Daima

Wagoma kupisha mradi wa bwawa

WAKAZI wa vijiji vya Bwirachini na Kiburungo Kata ya Selembala Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini wamegoma kuondoka kwenye makazi yao kupisha mradi wa bwawa la kufua umeme la Kidunda...

 

10 years ago

Habarileo

Machinga wagoma kuhama Jangwani

WAFANYABIASHARA ndogo ndogo maarufu kama ‘machinga’, waliohamishia biashara zao katika eneo la Jangwani wanaendelea na ujenzi wa vibanda pamoja na agizo la serikali kusisitiza kuwa wanapaswa kuhama eneo hilo.

 

5 years ago

Michuzi

UJENZI MRADI MKUBWA ENEO LA MAEGESHO YA NDEGE UWANJA WA NDEGE WAPAMBA MOTO ZANZIBAR

Kazi ya ujenzi wa mradi mkubwa wa eneo la maegegesho ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar zimeanza kupamba moto baada ya kusita kwa muda mrefu.

Harakati za umwagaji wa zege katika sehemu za kupakia na kushukia abiria ziko katika hatua nzuri chini ya wahandisi wa kampuni ya kimataifa ya CRJ kutoka nchini China wakisaidiwa na wahandisi na washauri wazalendo waliobobea kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere wa Dar es Salam.

Makamu wa Pili wa...

 

11 years ago

Dewji Blog

Breaking News: Wakazi wa Kurasini wafunga barabara kwa muda!

DSC_0457

Baadhi ya wakazi wa Mivinjeni Kurasini wakiwa na mabango katikati ya Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam hivi sasa, zenye ujumbe wa malalamiko ya kudai kulipwa  fidia zao ili kupisha mradi wa ujenzi wa bandari kavu kwenye eneo hilo.

DSC_0471

DSC_0472

DSC_0476

HABARI KAMILI ITAKUJIA HAPO BAADAE KIDOGO..!

DSC_0458

Baadhi ya magazri na mabasi yakigeuza yalikotoka.

DSC_0459

Gari lililokuwa likielekea kwenye maonyesho ya Sabasaba likizuiwa na wakazi wa eneo hilo.

DSC_0461

Mabasi yakizuiwa kupita.

DSC_0463

Baadhi ya waanawake wa eneo hilo wakimzuia...

 

11 years ago

Habarileo

Wakazi Pugu watakiwa kuhama

WIKI moja baada ya gazeti hili kuandika kuhusu hatari ya kupata magonjwa, ikiwemo kipindupindu inayowakabili wakazi wanaoishi karibu na dampo la Pugu Kinyamwezi na hatua ya kula kwenye chandarua walioianzisha kupunguza kero ya inzi, uongozi wa Jiji la Dar es Salaam umezungumzia hali hiyo.

 

9 years ago

StarTV

Wakazi wa mabondeni wapewa siku 14 kuhama

Serikali imesitisha kazi ya ubomoaji nyumba za wakazi wanaoishi maeneo ya mabondeni katika bonde la Mto Msimbazi jijini Dar Es Salaam kwa muda wa siku 14 ili kuwapatia nafasi ya kuondoka kwenye maeneo hayo kwa hiari.

Kazi hiyo ya kubomoa nyumba na vibanda vilivyojengwa kinyume cha sheria na maeneo oevu yasiyoruhusiwa kwa ajili ya makazi ya binadamu ilianza Novemba 18 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi na Mipangomiji namba 8 ya mwaka 2007 kifungu cha 30 imeleza kuwa hairuhusiwi wananchi...

 

11 years ago

Habarileo

Maegesho ya magari Dar sasa kusimamiwa na Jiji tu

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam imezinyang’anya rasmi Manispaa majukumu ya kusimamia maegesho ya magari na imefuta vibali vyote vya maegesho vilivyotolewa na mamlaka hizo. Hatua hiyo imekuja baada ya Kamati ya Ushauri Mkoa wa Dar es Salaam (RCC) kuagiza halmashauri ya Jiji kufanya kazi hiyo baada ya kubaini halmashauri za Ilala, Kinondoni na Temeke, kisheria hazikupaswa kusimamia maegesho ya magari.

 

Share

Magazeti ya Leo

Stay updated, Sign up

Habari za Mikoani