CUF yatangaza kuigomea polisi
Chama cha Wananchi (CUF) kimesema uamuzi wa Jeshi la Polisi kuzuia misafara ya wagombea urais wakati wa kuchukua na kurejesha fomu batili, kinyume na Katiba ya nchi na sheria ya vyama vya siasa, na unalenga “kuionea huruma CCM†baada ya kufunikwa na vyama vinavyounda Ukawa.
Mwananchi
Habari Zinazoendana
10 years ago
Vijimambo05 Jun
CUF yatangaza wagombea ubunge, uwakilishi.
![](http://www.ippmedia.com/media/picture/large/CUF-5June2015.jpg)
Chama cha Wananchi (CUF) kimetangaza majina ya wagombea ubunge na uwakilishi walioteuliwa na Baraza Kuu la chama hicho.
Baraza hilo lilikutana juzi jijini Dar es Salaam na kuchambua majina ya wagombea waliopitishwa kwenye kura za maoni katika majimbo mbalimbali nchini.
Wakati majina hayo yakitangazwa, baadhi ya wafuasi wa chama hicho wamelalamikia uteuzi huo kuwa haukuwa huru na haki.
Aidha, katika Jimbo la Mkanyageni, Pemba, wanachama wa chama hicho kwenye kura ya maoni ‘walimtema’ Mbunge wao...
10 years ago
Dewji Blog04 Jul
CUF yatangaza kuuvunja muungano wa Ukawa Ikungi
Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Ikungi na ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza kuu la uongozi Taifa,Bwana Athumani Henku akizungumza na mwandishi wa habari hizi(Picha Na Jumbe Ismailly).
Na Jumbe Ismailly,Ikungi
CHAMA Cha Wananchi (CUF) Wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida kimesema kitaandika barua kwenda CUF Makao makuu kuomba kuvunja masharti kwenye wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida yaliyofikiwa katika kikao cha pamoja cha vyama vilivyopo kwenye umoja wa Ukawa kuhusu kuachiana majimbo ya uchaguzi...
9 years ago
StarTV07 Nov
NEC yatangaza idadi ya uteuzi wa viti maalumuCCM, CHADEMA, CUF
Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC imetangaza idadi ya jumla ya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu kutoka vyama vya siasa vya CCM, CHADEMA na CUF. Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu mkurugenzi wa uchaguzi Emmanuel Kawishe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa Ibara ya 66 kifungu cha kwanza b na ibara ya 78 ya katiba ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ikisomwa kwa pamoja na kifungu cha 86 A cha sheria ya uchaguzi sura ya 343, Tume imepewa...
11 years ago
Tanzania Daima30 Jan
Polisi yatangaza vita Simiyu
JESHI la Polisi mkoani Simiyu limetangaza vita dhidi ya watu wanaojihusisha na mauaji ya vikongwe. Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya mfanyabiashara maarufu mjini Bariadi, Hidaya Sayi (38) kuuawa...
10 years ago
Habarileo13 Apr
Polisi wafuta mkutano wa CUF
POLISI katika Mkoa wa Kaskazini Unguja wamezuia mkutano wa hadhara wa Chama cha Wananchi (CUF) ambao ulikuwa ufanyike katika Jimbo la Kitope kwa maelezo kuwa haukupata kibali cha jeshi hilo.
10 years ago
Mwananchi02 May
Polisi yazuia mkutano wa CUF Songea
10 years ago
Mtanzania27 Feb
Washtakiwa CUF wawazidi ujanja polisi
Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam
HATI ya kuwafutia mashtaka wafuasi 30 wa Chama cha Wananchi (CUF) waliotakiwa kuunganishwa katika kesi moja na Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba, imezua sintofahamu baada ya wafuasi hao kutoweka.
Wafuasi hao waliotakiwa kuachiwa na kukamatwa tena walitoweka jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Emilius Mchauru, baada ya kukubali maombi ya kuwaachia huru yaliyowasilishwa na DPP.
DPP aliwasilisha hati ya kuomba...
9 years ago
Habarileo15 Sep
Mbunge wa CUF apongeza NEC, Polisi
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Jeshi la Polisi mjini Lindi mkoani Lindi imepongezwa kwa utendaji wake wa kazi kwa kufuata taratibu na sheria kwenye kampeni za uchaguzi zinazoendelea wakati huu.
10 years ago
StarTV28 Jan
Polisi yatawanya wafuasi wa CUF kwa mabomu.
Na Glory Matola,
Dar es Salaam.
Jeshi la Polisi limelazimika kulipua mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Wananchi CUF waliojiandaa kuandamana hadi Viwanja vya Zakhiem Mbagala jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya baadhi ya wafuasi wake huko Zanzibar.
Pamoja na mabomu hayo, Jeshi hilo pia lilimkamata Mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahimu Lipumba, baadhi ya wanachama na mwandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo na kupelekwa kituo...